Wednesday, August 29, 2012

TASAF awamu ya tatu

J.K AZINDUA AWAMU YA TATU YA TASAF  KWENYE UWANJA WA JAMHURI MJINI DODOMA.

AWAMU YA TATU YA TASAF INAJIPAMBANUA KAMA “MPANGO WA TAIFA WA KUNUSURU KAYA MASKINI ZILIZO KATIKA MAZINGIRA HATARISHI”
 HABARI KATIKA PICHA 
Umati wa Wananchi wa Manispaa ya Dodoma waliojitokeza kwenye uzinduzi wa awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF leo hii.  
Rais Kikwete akiwasili uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma maalumu kuzindua awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF.

Rais Kikwete akiambatana na viongozi wengine kwenda kuangalia Maonesho ya shughuli za wajasiriamali wadogo waliowezeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF  yaliokwenda sambamba na uzinduzi wa awamu ya tatu ya TASAF.
 Rais Kikwete akikagua mradi wa upandaji miti ya matunda na vivuli wa kikundi cha wazee cha Chiwene cha Manispaa ya Dodoma wakati wa sherehe za uzinduzi wa awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF.
Rais Kikwete akiangalia bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali wa kikundi cha Tuamke cha Ilala Dar es salaam kinachojihusisha na utengenezaji wa chaki na sabuni za maji wakati wa sherehe za uzinduzi wa awamu ya tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF Mjini Dodoma 
Rais Kikwete akikagua mradi wa ufugaji kuku chotara wa kikundi cha wajane cha Mamira Babati kilichowezeshwa na  Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya TASAF Mjini Dodoma 
Rais Kikwete akikagua nguo zilizoshonwa na kikundi cha Wazee cha Juhudi kutoka Manyara kilichowezeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya TASAF Mjini Dodoma
Habari na Dodoma Fm 98.4
  

0 comments:

Post a Comment